TUJIKUMBUSHE
Tanzania Tanzania, nakupenda kwa moyo wote,
Nchi yangu Tanzania, jina lako ni tamu sana
Nilalapo nakuwaza wewe, niamkapo ni heri mama wee
Tanzania Tanzania, nakupenda kwa moyo wote.
Tanzania Tanzania, ninapokwenda safarini,
Kutazama maajabu, biashara nayo makazi,
Sitaweza kusahau mimi, mambo mema ya kwetu hakika
Tanzania Tanzania, nakupenda kwa moyo wote.
Tanzania Tanzania, watu wengi wanakusifu,
Siasa yako na desturi, ilituletea uhuru
Hatuwezi kusahau sisi, mambo mema ya kwetu hakika
Tanzania Tanzania, nakupenda kwa moyo wote.
Tanzania Tanzania, Kaaribu wasio kwao,
Wenye shida na taabu, hukimbizwa na walowezi
Tanzania yawakaribisha, mpigane kiume chema wee
Tanzania Tanzania, heri yako kwa mataifa
Tanzania Tanzania, watu wako ni wema sana
Nchi nyingi zakuota, nuru yako hakuna tena
Na wageni wakukimbilia, ngome yako imara kweli wee
Tanzania Tanzania, Mola awe nawe daima